Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makonda awagusia waliotajwa na Magufuli

31221 Magufulipic RC Dar es Salaam, Paul Makonda

Wed, 12 Dec 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Baada ya juzi Rais John Magufuli kusema kuna wafanyabiashara wanaoagiza mizigo kutoka nje kwa niaba ya wenzao kisha kukwepa kodi, mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kazi kubwa inaendelea kufanyika ili kukabiliana nao.

Juzi, Rais alisema kuna wafanyabiashara wanaoingiza makontena kutoka nje kwa niaba ya wenzao, lakini hawalipi kodi hivyo kuikosesha Serikali mapato.

“Wapo wawili, mmoja jina lake linaishia na agency na mwingine lina o mwishoni. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam upo na TRA ipo, hamjui hili?” alihoji Rais Magufuli.

Juhudi za kuwapata wasemaji wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), mpaka tunakwenda mitamboni ili kupata ufafanuzi kuhusu taarifa alizonazo Rais hazikuzaa matunda.

Kuhusu wafanyabiashara wanaokwepa kodi kwa kuwatumia wamachinga, mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo (JWK), Philimon Chonde alisema wameshalifikisha suala hilo TRA mara kadhaa hivyo linahitaji ufuatiliaji.



Chanzo: mwananchi.co.tz