Leo JNICC mkuu wa mkoa wa Dar, Amos Makalla akiwa kwenye kongamano la nishati ya gesi ya kupikia linalodhaminiwa na Taifa Gas ameongelea changamoto ya maji Dar mbele ya Rais Samia.
Mamlaka ya hali ya hewa ilishatabiri, kwamba kutakuwa na kipindi kirefu cha ukame, kwahiyo ni kwamba chanzo cha ukosefu wa maji ni kudra za mwenyezi Mungu na wala sio ilani ya chama cha mapinduzi maana huwezi ilani ikataja ikaleta mvua kwa hiyo haya ni mambo ambayo yako nje ya uwezo wetu.
Hivi wale waarabu wa jangwani wangekuwa wanasubiri kudra za Mungu si wangekuwa wamekufa kwa kiu na ukame! Kama kupatikana maji safi ni nje ya uwezo wenu mtupishe maana hatutayapata mpaka tunakufa.