Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Majina ya waliofariki ajali ya basi Katavi haya hapa

Image 76.png Majina ya waliofariki ajali ya basi Katavi haya hapa

Fri, 10 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Majina ya watu saba kati ya tisa waliofariki katika ajali ya basi la Komba’s iliyotokea katika mlima Nkondwe uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi yametajwa na Mganga Mkuu Wilaya ya Tanganyika, Dk Alex Mrema.

Mjina ya marehemu hao ni pamoja na Beka Mashaka (8), Edigar Gilidas (1.5), Anisia Kapandila (52), Toa Nzikwi (30), Eva Sylvanus (40), Eliud Mashaka (10), na Anthonia Kapandila (27), huku miili ya marehemu wawili ikiwa haijatambuliwa.

Katika ajali hiyo, watu wengine 30 walijeruhiwa huku Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Ali Makame akisema chanzo cha ajali hiyo ni kufeli kwa breki na kusababisha basi hilo kukosa mwelekeo na kuporomoka bondeni.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko alisema serikali imeguswa na ajali hiyo na akatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa waliopoteza maisha, huku akisisitiza madereva kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live