Mon, 1 Mar 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya situ tatu mkoani Katavi ambapo pia atazindua kitabu cha mwongozo wa uwekezaji katika mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera amebainisha hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo.
RC Homera amesema Majaliwa atawasili mkoani humo Jumanne, ambapo baada ya ziara hiyo atazindua kitabu hicho.
Aidha, ameeleza kuwa viongozi wa serikali wa mkoa humo, wawekezaji na wadau watafanya ziara ya kutembelea maeneo ya uwekezaji na vivutio vya utalii vilivyopo Ziwa Tanganyika na Hifadhi ya Taifa ya Katavi.
Chanzo: habarileo.co.tz