Wed, 27 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali inaendelea na uimarishaji wa viwanja vya ndege nchini, ikiwmao kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Msalato jijini Dodoma.
Amesema kiwanja hicho kitaunganisha safari za ndani ya nchi na mikoa ya pembezoni pamoja na baadhi ya mataifa ya nje.
Amesema kiwanja hicho kimefikia asilimia 54.01 na majengo yake yamefika asilimia 19.85 na ujenzi unatarajiwa kukamilika Novemba mwaka 2025.
Majaliwa amesema hayo leo machi 26,2024 wakati wa kupokea ndege mpya aina ya Boeing 737 Max ya ATCL iliyotokea Marekani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live