Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mahagama azungumzia wizara ilivyowasaidia vijana 18,800

69412 Mhagama+pic

Fri, 2 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Morogoro. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu  nchini Tanzania, Jenista Mhagama amesema wizara hiyo imewasaidia vijana 18,800 wa  halmashauri za wilaya 88  kupata mafunzo ya teknolojia ya  kitalu nyumba ili waweze kujiajiri.

Mhagama ametoa kauli hiyo leo  Alhamisi Agosti Mosi, 2019 mkoani Morogoro katika ufunguzi wa maonyesho  ya 29 ya Nanenane Kanda ya Mashariki.

Amesema jambo hilo linawezekana kufanyika nchi nzima, kuna uhakika wa kuwa moja ya fursa za ajira kwa vijana wengi.

Amebainisha kuwa wataendelea kutoa mafunzo  katika sekta ya ufugaji wa samaki  kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

‘’Sekta za kilimo, mifugo na uvuvi vinaweza kuwa ajira mbadala  kwa  maisha ya kijana wetu wa Kitanzania hivyo lazima tuwawezeshe katika kila hali na hatua mbalimbali,” alisema waziri huyo.

Kuhusu wakulima, Mhagama amesema wataendelea  kuhamasisha  matumizi ya zana bora za kilimo kama  matrekta,  mashine za kupandia na  kuvunia mpunga  pamoja na za   kupukuchua  mahindi.

Pia Soma

 

Chanzo: mwananchi.co.tz