Fri, 14 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge leo June 14,2024 amemuapisha Petro Magoti Itozya (aliyekuwa Msaidizi wa Rais upande wa siasa), kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.
Uapisho umefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani iliyopo Kibaha na kuhudhuriwa na Wakuu wa Wilaya wengine wa Wilaya za Pwani, Viongozi wa Dini na Serikali na Wageni wengine waalikwa.
Itakumbukwa Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alimteua Petro Magoti kuwa DC wa Kisarawe June 06,2024 akichukua nafasi ya Fatma Almas Nyangasa ambaye amehamishiwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kondoa .
Chanzo: www.tanzaniaweb.live