Thu, 24 Oct 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Mbeya. Jeshi la Magereza mkoani Mbeya limekiri kudaiwa Sh191.9 milioni za maji ikiwa ni ankara ya mwaka 2012 hadi 2015.
Akizungumza na Mwananchi mkuu wa Magereza mkoani Mbeya, Mathias Mkoma amesema mwaka 2012/13 walikuwa na deni la Sh68.5 milioni, mwaka 2013/14 lilikuwa Sh123.4 milioni, kubainisha kuwa zitalipwa wakati wowote.
Oktoba 23, 2019 mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mkoa wa Mbeya, Ndele Mengo alitoa taarifa za wadaiwa sugu wa taasisi za Serikali likiwemo jeshi hilo.
Chanzo: mwananchi.co.tz