Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magazeti Jumatatu, Julai 19: Mama mjamzito miongoni mwa wahanga wa mkasa Siaya

89201da8866ec290 Magazeti Jumatatu, Julai 19: Mama mjamzito miongoni mwa wahanga wa mkasa Siaya

Mon, 19 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Magazeti ya Jumatatu, Julai 19, yameripotia kuhusu mkasa wa trela kulipuka katika kaunti ya Siaya.

Magazeti haya pia yameguzia siasa ambapo urithi wa Rais Uhuru Kenyatta umepewa uzito.

1. People Daily Gazeti hili limeripotia kuhusu watu 13 ambao waliangamia Jumapili, Julai 18, baada ya trela ambayo walikuwa wanachota mafuta kulipuka moto.

Kisa hicho kilitokea eneo la Malanga kwenye barabara kuu ya Kisumu-Busia.

Kulingana na mashahidi, moto huo ulichochewa na mlingoti wa stima ambapo trela hiyo iliangukia baada ya kujaribu kukwepa kugongana na lori iliyokuwa inasafirisha maziwa.

Ripoti zinadai kuwa wahanga walikuwa wanajuana na walikulia katika kijiji kimoja.

Vijiji vilivyoathirika ni Mutumbu, Sirunga, Lundha, Mwadi, Osodo na Nyabeda.

2. Daily Nation Kulingana na Daily Nation, Rais Uhuru Kenyatta ameshindwa kuchagua mrithi wake bora.

Read also

Mwili wa Mwimbaji Wanjaro Jr Aliyeripotiwa Kutoweka Wapatikana Bwawa la Masinga

Huku akijaribu kutimiza ajenda kuu nne ya maendeleo, rais analimbikiziwa presha ya kumtangaza mrithi wake 2022.

Huku naibu wake akipata umaarufu Mlimani, haijabainika bayana iwapo Uhuru atamuunga mkono kulingana na ahadi aliyomupa 2013 wakati walitafuta urais pamoja.

Pia mwingine kwenye rada ni kiongozi wa ODM, Raila Odinga ambaye alifikia makubaliano na Uhuru miaka mitatu iliyopita.

Bila msingi wa muafaka wao wa 2018 kuwekwa hadharani, wengi wana imani kuwa siasa za 2022 zilichochea handisheki.

Rais pia anaripotiwa kukumbana na usaliti kutoka kwa wandani wake wa karibu ambao wengi wao wamekimbilia katika kambi ya Ruto, ambaye alitofautiana Uhuru tangu handisheki.

3. Taifa Leo Taifa Leo pia limeripotia mkasa wa Siaya ambapo watu 13 walipoteza maisha yao.

Gazeti hili limetaja mapuuzi ya Wakenya kwenye visa vinavyhusiana na trela ya mafuta kuanguka.

Huku mikasa ya awali mamia wakipoteza maisha yao, gazeti hili linajaribu kuliza Wakenya watajifunza lini?

Miongoni mwa walioangamia kwenye mkasa wa Siaya ni mama mjamzito na mwingine aliyekuwa amebeba mtoto mgongoni.



Read also

Magazeti Ijumaa: Babu wa Miaka 93 Afunga Ndoa na Kipusa wa Miaka19

Moto huo ulilipuka baada ya mmoja wa wakazi kufungua tanki ili mafuta yaanze kumwagika na wachote.

4. The Standard Gazeti hili limeguzia aibu ya Jubilee kupoteza kiti cha Kiambaa.

Maafisa wa chama hicho tawala walisutwa na wabunge wa Kieleweke kwa kusajili matokeo duni baada ya kuongoza kampeni.

Wabunge hao wanataka katibu mkuu wa chama cha Jubilee, Rafael Tuju na naibu mwenyekiti David Murathe wajiuzulu kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Mgombea wa Jubilee katika uchaguzi huo mdogo, Kariri Njama alipoteza kwa mwaniaji wa United Democratic Alliance (UDA) John Wanjiku ambaye alitangazwa mshindi na kura 21,773, Njama alikuwa wa pili na kura 21,263.

5. The Star Wanasiasa wa Kieleweke mrengo katika chama cha Jubilee wamewalaumu maafisa wa chama hicho kwa kupoteza uchaguzi mdogo wa Kiambaa.

Uongozi wa chama hicho unakashifiwa kwa kutumia mbinu finyu ambao ulishuhudia chama hicho kikinyoroshwa na UDA.

Sasa wanawataka maafisa hao wajiuzulu.

READ ENGLISH VERSION

Read also

Kangogo Achezea DCI Karata na Habari Zingine Zilizotamba Wiki Hii

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke