Dodoma. Nyumba 109 katika kijiji cha Igandu Stesheni Wilaya ya Chamwino Mkoa wa Dodoma zimesombwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo.
Akizungumza na Mwananchi leo Alhamisi Februari 6, 2020 mwenyekiti wa kijiji hicho, George Yona amesema nyumba zimesombwa na maji kuanzia Februari 2, 2020 hadi usiku wa kuamkia leo.
Yona amesema mbali na wananchi hao kukosa makazi, hawana chakula.
“Wakazi wa nyumba 109 hawana makazi wanaishi kwa majirani walionusurika katika mafuriko hayo, wapo wengine hawana hata sehemu ya kujihifadhi, tunaomba Serikali itusaidie,” amesema Yona.
Amebainisha kuwa walitoa taarifa kwa uongozi wa kata ya Igandu pamoja na tarafa lakini hakuna juhudi zozote zilizochukuliwa.
Gipson Makonde, mkazi wa kijiji hicho amesema familia yake ya watu wanane haina pa kuishi baada ya nyumba kubomoka.
Pia Soma
- Serikali ya Tanzania yaagiza tani 225,000 za mbolea
- Hospitali ya Mloganzila yatajwa upungufu wa watumishi
- Rais Magufuli ayashukia mabaraza ya ardhi
- Askofu Maboya asema watafunga siku saba kuwaombea waliokufa kongamano wa Mwaposa