Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mafundi sanifu, wahandisi wapewa somo

Sun, 26 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elius Mwakalinga amewapa mbinu mafundi sanifu na wahandisi  nchini itakayosaidia kushindana na wenzao  kwenye soko ajira la Jumuiya Afrika Mashiriki (EAC).

Mwakalinga amesema mbinu hiyo ni  pamoja kujijenga uwezo na kufanya kazi kwa  bidii kwa kutumia fursa zilizopo za utekelezaji wa miradi ya maendeleo, jambo alilodai kitakuwa dawa na kinga kwa Watanzania.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Mei 24, 2019 katika kongamano la pili la mwaka la mafundi sanifu lililoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB), na kufanyika jijini Dar es Salaam.

Amebainisha kuwa kuna presha inakuja kwamba EAC ikiwa kitu kimoja kutakuwa na changamoto ya ajira, wote watashindanishwa.

“Mchakato wa kufikia hatua hiyo bado haujasainiwa. Tunamshukuru Rais John Magufuli maana tungejikuta  tuna wageni hapa nchini, "amesema Mwakalinga.

Ametumia fursa hiyo kuhimiza upendo kati ya mafundi sanifu na wahandisi akitaka wapendane badala ya kubaguana kwamba kila mmoja anamtegemea mwenzake katika utekelezaji wa majukumu.

Pia Soma

“Tuwe na umoja na tupendane ndio jambo la msingi. Tujenge imani ya kuaminiana kwa kila mmoja wetu na tuwe wavumilivu," amesema Mwakalinga.

Mwenyekiti wa  bodi ya ERB,  Profesa Ninatubu Lema alimweleza Mwakalinga kuwa bado kuna changamoto ya uhaba ya mafundi sanifu na tangu waanze kusajiliwa mwaka 2014 wamefikia 112.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz