Watu wanne katika Kijiji cha Rusumo wilaya ya Ngara mkoani Kagera wamefariki dunia kwa ajali ya moto na wengine saba kunusurika baada ya nyumba waliyokuwa wamelala kuungua moto usiku wa kuamkia leo Aprili 25, 2024.
Watu wanne katika Kijiji cha Rusumo wilaya ya Ngara mkoani Kagera wamefariki dunia kwa ajali ya moto na wengine saba kunusurika baada ya nyumba waliyokuwa wamelala kuungua moto usiku wa kuamkia leo Aprili 25, 2024. Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Kagera Kamishna Msaidizi Zabron Muhumha, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa chanzo cha tukio hilo ni kuwa chumba hicho walichokuwa wamelala kilikuwa na madumu ya petroli.