Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Madiwani walia tembo, simba kuvamia makazi ya wananchi

Madiwani walia tembo, simba kuvamia makazi ya wananchi

Mon, 17 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Morogoro. Temba na simba wanaotoka Hifadhi ya Taifa Mikumi mkoani Morogoro wamevamia  mashamba na makazi ya wananchi wa Wilaya ya Mvomelo  na kuzua taharuki sambamba na kuharibu mazao.

Akizungumza leo Jumamosi Februari 15, 2020 katika kikao cha bajeti cha baraza la madiwani Wilaya ya Mvomelo Diwani wa Doma, Elimu Kisugulu amesema wanyamapori hao wamekuwa wakionekana kuanzia saa 10 jioni.

“Ni kama wananchi tunawalimia wanyama hawa kwa sababu wanaharibu mazao yetu, hata wananchi sasa wanaogopa kutembea jioni. Ikifika saa 10 kila mtu amejifungia nyumbani kwake,” amesema diwani huyo.

Amebainisha jitihada zinazofanywa na Serikali kuwadhibiti wanyama hao hazitoshi, sasa wananchi wanataka kuonana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla.

Amesema miaka ya nyuma kila kijiji kilichopakana na hifadhi kulikuwa na askari wa wanyamapori, kwamba kwa sasa askari wapo watatu katika wilaya nzima ya Mvomelo.

“Niombe kwa ridhaa yako na wajumbe tulipofikia tukamuone Kigwangalla pengine tunaweza kupata muafaka kinyume na hapo tutaendelea kuzika watu kila mwaka hapa tayari tumezika wakazi wa kijiji cha Mangae, Mahalaka na Mtipule,” amesema diwani huyo.

Pia Soma

Advertisement
Diwani wa Lubungo,  Hamidu Zuberi amesema,” miaka ya nyuma wanyama kama tembo walikuwa wakipita mwezi Aprili hadi Julai, lakini kipindi hiki wamegeuza maeneo hayo kama sebule. Wanyama wanaweka makazi jambo linalotupa wasiwasi kwani watu wanapoteza maisha.”

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Jonas Van Zeeland amemuagiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Florent Kyombo kutekeleza maagizo na kuandaa taarifa ya jitihada zilizochukuliwa, walipokwama ili aweze kufahamu maeneo yanayohitaji msaada.

Chanzo: mwananchi.co.tz