Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Madereva waungana kupinga ukatili wa Kijinsia

EBFC206E 91D9 4079 B2DB EB63DC13B583.jpeg Madereva waungana kupinga ukatili wa Kijinsia

Sat, 14 Jan 2023 Chanzo: dar24.com

Chama cha madereva wa Bajaji Manispaa ya Iringa wamehimizana kuacha kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa abiria wao na kwamba hawatamvumilia mtu yeyote ambaye atakiuka mpango huo.

Mwenyekiti wa chama hicho, Melabu Kihwele akiongea wakati wa ziara ya kuzungukia maegesho ya Bajaji kwa nyakati tofauti alisema uongozi wao  umedhamiria kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Amesema, wao Kama wanaumoja wa Bajaji Mkoani Iringa wanayo dhamira ya dhati ya kuunga mkono juhudi za Serikali za kupinga vitendo vya ukatili kwa Watoto na wanawake, ambavyo kwa siku za hivi karibu vimezidi kuongezeka.

Alisema kuwa Dereva Bajaji yoyote atakaye baka au kulawiti hawatamfumbia macho kwa kuharibu taswira yao kama ambavyo imetokea kwa siku za karibuni kwa Dereva Bajaji wa Manispaa ya Iringa amefungwa miaka 30 jera kwa kosa la ukatili wa kijinsia.

Chanzo: dar24.com