Madereva pamoja na abiria wa magari yaendayo Mikoa ya Kusini wameomba serikali kutumia jina la Rais Samia kwenye stendi ya magari ya Kusini iliyopo Kijiji cha Mwandege wilayani Temeke.
Madereva hao wamesema wao kama wadau wa usafirishaji wanapitia changamoto mbalimbali kuomba Rais kuwasaidia ili kuweza kufanya kazi zao katika mazingira mazuri zaidi.
Hali hiyo imekuja mara baada ya madereva hao kufika kwenye stendi hiyo ya Mwandege na kuomna uongozi wa halmashauri kusimamia ujenzi wa kituo hicho kwani itakuwa ni rahisi kwao kufanya kazi katika eneo hilo.
Haya yanajiri baada ya iliyokuwa Stendi ya Mabasi yaendayo Mikoa ya Kusini iliyokuwa Mbagala Rangi Tatu kuhamishiwa Kijichi kutokana na ufinyu wa eneo hilo.