Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Machinjio wilayani Mvomero mbioni kuanza kutumika

Machinjipicc Data Machinjio wilayani Mvomero mbioni kuanza kutumika

Sun, 23 Jan 2022 Chanzo: www.mwananchi.co.tz

Machinjio ya kisasa kwa mifugo ya Nguru Hills Ranch Ltd yataanza kutumika Machi Mosi mwaka 2022.

Katika machinjio hayo yaliyopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro kwa siku watakuwa wakichinjwa ng’ombe 100 na mbuzi  1,000 na kuchochea ukuaji wa uchumi na ajira.

Mradi wa machinjio hayo ya kisasa ni upo chini ya ubia wa Serikali kupitia Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF ),  Eclipse Investiment (LLC) na kampuni ya Busara Investment (LLP).

Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji wa PSSSF , Fortunatus Magambo amesema hayo  mbele ya wahariri wa vyombo vya habari  waliotembelea  mradi wa  machinjio ya kisasa ya Nguru.

Amesema mradi huo ulianza mwaka 2018  lakini ugonjwa wa Uviko-19 ulipoanza ulisababisha mashine zilizoangizwa kutoka nje ya nchi kuchelewa kuwasili nchini  wakiwemo na wataalamu wa kuzifunga hadi kufikia Julai 2021.

Amebainisha kuwa mifumo ya maji , umeme , ufungaji wa mashine za kuchinjia na mifumo ya kupoozea vimekamilika kwa asilimia  kubwa.

“Uzalishaji wa kuchinja  ng’ombe na mbuzi kuanzia Machi utaajiri   wafanyakazi 300 na 120 watakuwa wa kudumu. Tupo katika hatua ya mwisho kila kitu kimeisha, tutakachofanya kuanzia Januari  24, 2022 tutaanza kuleta ng’ombe wa kunenepesha kwa ajili ya kuchinja,” amesema.

Chanzo: www.mwananchi.co.tz