Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mabasi 10 yazuiwa kusafirisha abiria Tabora

Mabasi Tabora Mabasi

Mon, 27 Sep 2021 Chanzo: Wasafifm

Jeshi la polisi Mkoa wa Tabora limeendesha msako maalumu wa kuondosha magari yote mabovu ya kubeba abiria ndani ya stendi kuu ya mabasi mkoani Tabora .

Katika msako endelevu ambao umefanyika September 27 kuanzia majira ya saa kumi na moja alfajiri ukiongozwa na mkuu wa usalama barabarani mkoa wa Tabora SP. Gabriel Chiguma amesema mbali na kuondosha Magari yote mabovu yanayobeba abiria kwenda mikoani pia msako huo ndani yake umelenga kupunguza wimbi la ajali ambazo zimekuwa zikitokana na ubovu wa magari.

Aidha katika msako huo jumla ya magari 10 ya abiria yamezuiliwa kuendelea na safari zake mpaka yatakapo kamilisha matengenezo yaliyoelekezwa na Jeshi la Polisi ikiwemo ubovu wa mabodi, matairi, breki pamoja na mivujo ya mafuta katika sehemu za Injini.

Hata hivyo, abiria wamesema zoezi la magari kukaguliliwa ni muhimu kuwa endelevu kutokana na gari nyingi zimekuwa zikitumika na wamiliki barabarani hali kuwa ni mbovu.

Chanzo: Wasafifm