Tue, 15 Oct 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Buchosa. Mabaki ya mwili wa Magesa Biseko (12), aliyeliwa na mamba Oktoba 11, 2019 yamepatikana katika Ziwa Victoria.
Biseko, aliyekuwa akisoma darasa la sita shule ya Msingi Itabagumba aliliwa na mamba katika kijiji cha Bulyaheke B kata ya Bulyaheke wilayani Sengerema.
Akizungumza leo Jumatatu Oktoba 14, 2019 ofisa mtendaji wa kijiji hicho, Berenadetha Sandu amesema jitihada ya kupata mabaki ya mwanafunzi huyo zimefanywa na wavuvi na kuzikwa kijijini hapo.
Chanzo: mwananchi.co.tz