Thu, 8 Sep 2022
Chanzo: EATV
Watu 9 wamejeruhiwa usiku wa kuamkia leo Septemba 8, 2022, kwenye ajali iliyotokea katika eneo la Sakina jijini Arusha, baada ya lori lililokuwa limebeba shehena ya mahindi likitokea Arusha kuelekea Namanga kupoteza mwelekeo na kuzigonga daladala tatu.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Justine Masejo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, na kusema kwamba jeshi hilo linaendelea na uchunguzi ili kubaini sababu ya lori hilo kupoteza mwelekeo na kusababisha maafa hayo.
Aidha Kama Masejo amesema kuwa, majeruhi wa ajali hiyo wanapatiwa matibabu katika hospitali ya Mount Meru, mkoani humo.
Chanzo: EATV