Lori lenye tenki la mafuta imeanguka na kuwaka moto muda huu pembezoni mwa Barabara ya Morogoro katika maeneo ya Kimara Kibo jijini Dar es Salaam.
Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika na mpaka hivi sasa bado hakuna taarifa rasmi juu ya athari zilizosababishwa na ajali hiyo.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Dar es Salaam limefanikiwa kumefanikiwa kuzima sehemu ya moto wa lori la mafuta.
Updates:
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro amesema mpaka sasa hawajapa taarifa ya mtu yoyote kupoteza maisha katika ajali ya moto iliyotokea Kimara baada ya lori la mafuta kulipuka.