Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kupaka rangi, kujenga uzio Kinondoni lazima uwe na kibali

98857 Rangi+pic Kupaka rangi, kujenga uzio Kinondoni lazima uwe na kibali

Fri, 13 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imetilia mkazo sheria ya ardhi na upangaji miji ambayo inamtaka kila mkazi katika eneo lake anapotaka kufanya ukarabati wa nyumba yake, kupaka rangi ama kujenga uzio lazima awe na kibali kutoka halmashauri.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Machi 12, 2020  mkurugenzi wa manispaa ya Kinondoni,  Aron Kagulumjuli amesema  kibali hicho hakitolewi bure bali kinalipiwa, kwamba  kuhusu kiasi inategemea na aina ya ukarabati unaofanya.

Alitoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa na Mwananchi kuhusu mjadala ulioibuka katika mitandao ya kijamii kuhusu suala hilo, jinsi wengi waliochangia kuonekana kutoijua sheria hiyo.

“Ni kweli, mwananchi yoyote anayetaka kupaka rangi, kufanya marekebisho ama kujenga ukuta ni lazima apate kibali kutoka mamlaka ya upangaji miji ambayo ni halmashauri, huu ni utekelezaji wa sheria ambayo ipo muda mrefu,”  amesema.

Amesema kuwa watu wamezoea kufanya kazi kwa mazoea bila usimamizi wa sheria, kwamba sheria hiyo kwa sasa inatekelezwa.

Mkazi wa Kinondoni, Clemence Malya anayeishi Mikocheni amesema hana uelewa kuhusu sheria hiyo na alishangaa kuitwa serikali za mitaa kwa madai kuwa ameweka uzio wa nyumba yake bila kuwa na kibali.

Pia Soma

Advertisement
“Sikuwa nikijua kuwa kujenga ukuta lazima uwe na kibali kutoka halmashauri, ilitokea tu juzi wakati napaka rangi na kutengeneza ukuta wa  nyumba yangu uongozi wa serikali ukaja kuniuliza kuhusu kibali,  nilishangaa kwakuwa utaratibu huo ni mpya kwangu,” amesema.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz