Mon, 25 Jan 2021
Chanzo: habarileo.co.tz
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge amewataka wakazi wa jiji hilo kufika kwa wingi katika viwanja vya Mnazi Mmoja ili kupata ushauri na msaada wa mambo ya kisheria bila malipo.
RC Kunenge ameyasema hayo leo wakati akifungua maadhimisho ya wiki ya sheria katika Kanda ya Dar es Salaam yaliyoenda sambamba na maadhimisho ya Mahakama Kuu ya Tanzania kutimiza Miaka 100.
“Natoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaaam kujitokeza kwa wingi wakiwemo watendaji wa serikali na waajiri wote ili wapate suluhisho la matatizo mbalimbali ya kisheria ambayo uwa wanakutana nayo” amesema Kunenge.
Chanzo: habarileo.co.tz