MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge, amewataka wakazi wa Dar es Salaam, watakaopenda kuaga mwili wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, kufika uwanja wa Uhuru saa 12 asubuhi kesho.
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Aboubakar Kunenge, amewataka wakazi wa Dar es Salaam, watakaopenda kuaga mwili wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, kufika uwanja wa Uhuru saa 12 asubuhi kesho. Kunenge aliyasema hayo muda mfupi wakati viongozi mbali mbali wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, John Kijazi walipofika Uwanja wa Uhuru kukagua mandalizi yanayoendelea, ambapo mwili wa Mkapa utapelekwa ukitokea hospitali na wananchi watapata fursa ya kuaga kwa siku tatu mfululizo.