Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Korti yasema Nondo ana kesi ya kujibu

14045 Pic+nondo TanzaniaWeb

Mon, 27 Aug 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Iringa. Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa, imesema mwenyekiti wa mtandao wa wanafunzi wa vyuo vikuu, Abdul Nondo ana kesi ya kujibu.

Hakimu Liad Chamshama akitoa uamuzi leo Agosti 27, 2018 amesema ushahidi na vielelezo vilivyotolewa na Jamhuri katika kesi unaonyesha Nondo ana kesi ya kujibu.

Amesema Nondo anatakiwa kuthibitisha maelezo aliyoyatoa kwa ofisa wa polisi.

Katika kesi hiyo Nondo anashtakiwa kwa makosa mawili akidaiwa kutoa taarifa ya uongo kwa ofisa wa polisi wa kituo Mafinga akidai alitekwa na watu wasiojulikana, kosa analodaiwa kutenda Machi 7, 2018.

Pia, anashtakiwa kwa kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni.

Hakimu Chamshama amesema Nondo ana haki ya kujitetea kwa kiapo au bila kiapo. Pia, ana uhuru wa kupeleka mashahidi.

Wakili wa utetezi, Chance Luoga amesema mteja wake atajitetea kwa kiapo na atakuwa na mashahidi watano.

Mahakama imepanga Septemba 18 na 19, 2018 kuanza kusikiliza mashahidi wa upande wa utetezi.

Chanzo: mwananchi.co.tz