Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kimbunga kilichoikumba Arusha, Muongoza watalii aliyezama aendelea kusakwa

78160 Pic+arusha

Wed, 2 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arumeru. Vikosi vya uokoaji, vinaendelea kumtafuta Muongoza watalii, Samwel  Mhina (33)  pamoja na Mtumbwi  aliokuwa amepanda  baada ya jana jioni kuzama katika ziwa Momella  kutokana na kimbunga kilichoukumba mkoa wa Arusha.

Katika tukio hilo, watalii wawili na muongoza watalii mwingine mmoja, waliokolewa baada ya Ziwa hilo kuchafuka ghafla majira ya saa nane  na nusu mchana hadi saa 10 jioni.

Kamanda wa  Polisi wa Oparesheni mkoa wa Arusha Francis Joseph akizungumza leo Octoba 3 wakati zoezi la kumtafuta Mhina na Mtumwi likiendelea amesema kuwa tukio la uokoaji lilianza Jana jioni bila ya mafanikio.

"Hadi leo bado tunamtafuta  kijana huyu, mitumbwi iko kwenye maji kwa kuendelea kumtafuta huku wakitumia nyavu kutazama kama mwili umezama chini ya ardhi.. Jana jioni  watalii wawili pamoja na muongoza watalii mmoja waliokolewa wakiwa hai"amesema.

Afisa mwandamizi wa hifadhi ya Taifa ya  Arusha, Maria Kirombo amesema  katika tukio hilo Mitumbwi  miwili  ilikuwa ikifanya utalii katika ziwa hilo, kulikuwa na watalii wawili pamoja na waongoza watalii wawili ambao ni Alpha  Mosha 24 na  Samweli Mhina (33).

Amesema baada ya kimbunga kuvuma, Mtumbwi uliokuwa  ikiongozwa na samweli  ulizama ndipo alipoanza kuogelea na kupotezana na wenzake  na kuweza kupatikana yeye na wenzake watatu wakiwa hai.

Pia Soma

Advertisement
Maria alisema  kuwa ziwa Momela lina urefu wa mita kumi pia  pembeni kuna wanyamapori.

Mzazi wa kijana huyo ambaye bado hajapatikana  Geldat Mhina amesema kuwa taarifa ya tukio hilo aliipata akiwa katika hifadhi ya Manyara akiwa ni mfanyakazi wa hifadhi ya hiyo hivyo aliitwa ofisini  na kuja katika tukio hili.

"Natarajia mtoto wangu atapatikana akiwa hai au amekufa  tuendelee kumuomba mungu  afanikishe katika hili" amesema

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro   amewapa pole familia ya Mhina amewataka wananchi kuendendele kuwa na subra  kwa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama  vinafanyakazi na kufanya jitihada ya kumpata samweli na taarifa sahihi zitatolewa .

Chanzo: mwananchi.co.tz