Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kilo 400 za nyama zilizoharibika zateketezwa Arusha

Fri, 31 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Bodi ya Nyama  Tanzana, imeteketeza nyama ya ng’ombe kilo 400 na kumtoza faini ya Sh milioni moja   mfanyabiashara   Patrick Akyoo katika soko la Samunge baada ya kukutwa akiuza nyama iliyooza.

Akizungumza mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika soko la Samunge,   Kaimu Msajili wa bodi hiyo , Imani Sichalwe amesema nyama iliyokuwa inauzwa na mfanyabiashara huyo haikidhi viwango na sheria.

“Ili nyama iuzwe lazima ipigwe muhuri ambao unathibitisha kuwa nyama hiyo imepimwa na daktari na ni sawa kwa mtumiaji na haitaleta madhara kwa jamii, ”amesema

 

Sichwale amesema  mfanyabiashara huyo amevunja sheria za kuuza nyama ikiwamo kufanya biashara hiyo kwenye maeneo machafu, ikiwa siyo mara ya kwanza kwa sababu aliwahi kupewa onyo Mei 19, 2019 lakini amekaidi na kuendelea.

 “Tulipita mara ya kwanza tukatoa onyo kwenye bucha zote  sokoni hapa ambazo hazijakidhi vigezo ikiwemo hii wenzake walitii kasoro yeye hakutekeleza agizo letu akaendelea kuuza , iwapo atafungua tena tutaifungia leseni yake moja kwa moja,” amesema.

Pia Soma

Kaimu huyo amesema soko la Samunge lina maduka ya nyama yapatao 13 na moja ndilo lililokidhi vigezo vya uuzaji wa nyama kwa ulaji wa binadamu kama vile kuweka marumaru chini na juu ya ukuta.

Amesema jambo lingine ni kuwa na mashine za kukatia nyama na si magogo na nguo za muuzaji ziwe nyeupe na eploni yake iwe ya karatasi inayoweza kufutika na si kitambaa ,kofia na viatu vigumu maarufu kama gambuti.

Amesema mkoa wa Arusha wamekagua bucha zipatao 235 ikiwa zilizofungiwa ni 16 ambapo Samunge 11,Usariver  moja  kwa Aloyce mbili na Mto wa Mbu mbili kuanzia Mei 11,  2019.

Hata hivyo Afisa mfawidhi  kituo cha uchunguzi wa magonjwa  ya mifugo kanda ya kaskazini Dk Obedi Nyasebwa amesema nyama hiyo haikuchunjwa ni mzoga, kwani hata rangi ilikuwa tofauti na nyama nyingine.

Chanzo: mwananchi.co.tz