Walimu katika Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi, wametaja sababu za Elimu kushuka wilayani humo kuwa ni wazazi kutowapatia watoto muda mzuri wa kujisomea, tatizo la umbali wa shule na nyumbani lakini pia kitendo cha wazazi kutelekeza watoto kwa wazee wasiojiweza hivyo kuchangia aina ya malezi yasiyo bora.
Walimu katika Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi, wametaja sababu za Elimu kushuka wilayani humo kuwa ni wazazi kutowapatia watoto muda mzuri wa kujisomea, tatizo la umbali wa shule na nyumbani lakini pia kitendo cha wazazi kutelekeza watoto kwa wazee wasiojiweza hivyo kuchangia aina ya malezi yasiyo bora. Wakizungumza katika mdahalo wa nini kifanyike ili kukuza elimu wilayani Nachingwea, walimu wameeleza changamoto ya watoto kutembea umbali mrefu kutoka nyumbani kuelekea shule ambapo hata wafikapo nyumbani hupambana na kazi nyingi hivyo kushindwa kupata muda mzuri wa kujisomea.