Katavi. Rais wa Tanzania, John Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe kufanya upembuzi yakinifu ili kipande cha barabara ya Sitalike- Kibaoni mkoani Katavi chenye urefu wa kilomita 71 kujengwa kwa kiwango cha lami.
Kiongozi mkuu huyo wa nchi ametoa agizo hilo leo Jumatano Oktoba 9, 2019 wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Mlele katika mkutano hadhara uliofanyika kijiji cha Kibaoni.
Amesema Mkoa wa Katavi ni kati ya mikoa inayozalisha mazao mengi ya chakula na biashara, hivyo ni lazima barabara hiyo ijengwe kwa kiwango cha lami kuwasaidia wakulima kusafirisha mazao yao.
Magufuli leo alifungua barabara ya Kanazi-Kizi na Kibaoni inayounganisha mkoa wa Katavi na Rukwa yenye urefu wa kilomita 76.6 iliyojengwa kwa kiwango cha lami kwa Sh100.5bilioni