Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kafulila awajia juu wanaotafuna michango

96244 Kafulila+pic Kafulila awajia juu wanaotafuna michango

Wed, 19 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mbozi. Katibu tawala Mkoa wa Songwe, David Kafulila amewaagiza wakurugenzi watendaji wa halmashauri kuwachukulia hatua kali za kiutumishi watumishi wanaotafuna fedha za makusanyo kabla hawajachukuliwa hatua wao.

Kafulila ameitoa kauli hiyo leo, Jumanne Februari 18 mwaka huu katika kikao cha kamati ya ushauriano cha mkoa (RCC) kuwa halmashauri zinakwama kufikia malengo ya makusanyo kutokana na wakusanyaji hao kula fedha baada ya kuzikusanya badala ya kuziwasilisha benki.

"Wakusanyaji wa mapato ya halmashauri ni watumishi wa umma, wanatambua kuwa ulaji wa fedha za Serikali ni kosa ambalo linatosha kumfukuzisha kazi mtumishi husika kwa mujibu wa kanuni na kuchukua hatua nyinginezo za kisheria," amesema Kafulila.

Kafulila alitangaza kupiga marufuku kufanya majadiliano na watumishi aliodai ni wezi na kutoa siku saba hatua ziwe zimechukuliwa na wahusika hao wafikishwe Takukuru.

Aidha inadaiwa kuwa zaidi ya Sh200 milioni zipo mikononi mwa watendaji ambazo zimekusanywa kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ya halmashauri.

Mkuu wa wilaya Momba, Jumaa Said Irando amesema katika wilaya yake zaidi ya Sh63 milioni zipo mikononi mwa watendaji na kuwa orodha yake ameiwasilisha Takukuru.

Pia Soma

Advertisement


Chanzo: mwananchi.co.tz