Mkuu wa wilaya ya Monduli Joshua Nassary kwa kushirikiana na Vyombo vya ulinzi na usalama Pamoja na Maafisa wanyamapori wamemkamata Jangili wa wanyamapori ambaye inadaiwa amekuwa akishirikiana na watu wengine kufanya shughuli hiyo
Mtuhumiwa huyo wa ujangili amefahamika kwa jina la Gida Ally Jumanne ambapo amekamatwa akiwa na nyama ya Pundamilia huku akieleza kuwa yeye sio mwindaji haramu wa Wanyamapori bali hutumika kusafirishi nyama kwa kutumia pikipiki.
Kulingana na Afisa wanyamapori wa wilaya ya Monduli Isaack Urasa amesema mtuhumiwa huyo ana kesi nyingine mahakamani ya ujangili ambayo alifunguliwa mwaka huu kisha kupewa dhamana lakini bado hajakoma tabia hiyo.
Tazama Video Hapa Chini;