Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jafo azindua kampeni ya Watanzania kutopeana mikono

28518 DODOMA+PIC TanzaniaWeb

Fri, 23 Nov 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. 'Nakupenda, unanipenda, usinishike mkono' ni kampeni inayoanzishwa na Waziri wa nchi ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Seleman Jafo ili Watanzania waache kushikana mikononi.

Jafo amesema hayo leo Ijumaa Novemba 23, 2018 wakati akitoa neno la shukrani kwa hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati akifunga semina ya siku tatu kwa maofisa afya wa halmashauri na mikoa nchini iliyofanyika jijini Dodoma.

"Hii ni hatari sana hasa kwa viongozi, utakuta katika mkoa unaofanya ziara watu zaidi ya 40 wanakusubiri mnapeana mikono wakati kuna magonjwa ya kuambukiza, nataka tuwe tunapungiana mikono," amesema Jafo

Amesema viongozi ndiyo watakuwa waathirika namba moja kwani wanaokaa kwenye foleni hizo huwa wametoka maeneo mbalimbali bila kunawa lakini wanakimbilia kuwapa mikono viongozi.

Waziri huyo amesema tayari ameshazungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ili waone namna bora ya kuliweka jambo hilo kwa faida ya Watanzania.

Katika hatua nyingine, Jafo amesema watakaa pamoja na Waziri Ummy ili kupunguza mambo mengine ambayo yanatokana na mambo yasiyo ya lazima.



Chanzo: mwananchi.co.tz