Fri, 24 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoani Tabora limemkamata kijana mwenye umri wa miaka 25 anayetuhumiwa kujifanya askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wilayani Nzega, ambaye amekutwa na bastola bandia anayodaiwa kuitumia kwa kutisha watu na kujipatia kipato.
Wakati huo huo, jeshi hilo limemkamata mwanaume mwenye umri wa miaka 56 kwa tuhuma za kumfyatulia risasi mtoto wake kwa lengo la kutaka kumuua.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Richard amesema mzee huyo alifyatua risasi kutokana na mtafaruku uliojitokeza ndani ya familia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live