Wananchi wa eneo la Kitwiru mkoani Iringa wamelazimika kufunga barabara kwa muda, wakishinikiza kuwekwa kwa alama ya wavuka kwa miguu au matuta, kutokana na matukio ya ajali za mara kwa mara za watu kugongwa katika barabara hiyo.
Wakazi hao wamesema wanawaomba Wakala wa Barabara. Tanzania (TANROADS) kuweka tuta eneo hilo kwa kuwa kuna shule karibu na eneo husika huku mistari ya pundamilia ipo mbali na hapo.
Diwani wa Kata ya Kitwiru, Dk Hamza Mumuhehe alipoulizwa amesemea kwa mujibu wa maelezo ya TANROADS kitaalamu eneo hilo ni ngumu kuweka tuta kwa kuwa kuna kona na mlima badala yake wakaweka matuta karibukaribu.