Arusha. Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro amempandisha cheo sajenti Meshack Samson kuwa stafu sajenti na kumzawadia Sh1 milioni baada ya kukataa kupokea rushwa ya Sh10 milioni.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Desemba 22, 2019 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan Shana amesema askari huyo aliombwa kupokea Sh10 milioni ili afute tuhuma alizokuwa akizifuatilia.
"Tumewakamata watuhumiwa wawili wakishirikiana na Polisi wetu kutaka kumpa rushwa sajenti Meshack ili kumaliza kesi inayomkabili ndugu yao, hili jambo halikubaliki kabisa katika jeshi letu," amesema Shana.