IKIWA ni siku tatu tangu kuzinduliwa kwa utoaji wa hatimilki za ardhi kupitia programu ya Ardhi Kliniki Wilaya ya Ubungo mkoani Dar es Salaam, hati 283 zimeshatolewa na migogoro ya ardhi 69 imetatuliwa.
Mratibu wa programu hiyo ya urasimishaji katika Manispaa ya Ubungo, John Ilomo ameeleza hayo alipokuwa akizungumzia muitikio wa wananchi kuchukua hati zao.
"Mpaka sasa tumefanikiwa kutoa hati hizi hii inaonesha kuwa wananchi wameelewa na wameitikia wito kufika kwenye viwanja hivi kwa ajili ya kujipatia hati, hakika wananchi wameelewa kuwa serikali imewasogeze huduma,” amesema.
Amesema japokuwa kuna hali ya mvua, lakini mwitiko wa wananchi umekuwa mzuri wanajitokeza hali inayoonesha kuwa walikuwa na uhitaji wa huduma hiyo karibu.