Wed, 18 Sep 2019
Chanzo: mwananchi.co.tz
Tanga. Shule ya Sekondari Old Tanga nchini Tanzania inateketea kwa moto ulioanza leo mchana Jumatano Septemba 18, 2019.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Edward Bukombe amesema chanzo cha moto huo ulioteketeza chumba cha mikutano na cha kuhifadhi vifaa bado hakijafahamika
Jitihada za kuuzima moto huo zinaendelea kwa vikosi vya zima moto kuuthibiti moto huo ili usiendelee kusababisha madhara zaidi.
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa habari zaidi
Chanzo: mwananchi.co.tz