Mon, 19 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ghorofa lililokuwa linajengwa eneo la Marangu Sembeti Wilayani Moshi limeanguka asubuhi ya leo Disemba 19, 2022.
Kikosi cha uokoaji kimefika eneo la ajali kwa ajili ya kuwaokoa watu wanaosadikiwa kufunikwa na jengo hilo huku watu watano wakipoteza maisha.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Abbas Kayanda amethibitisha vifo hivyo na kueleza kuwa watu wengine kadhaa waliokuwa katika eneo hilo wameokolewa
Chanzo: www.tanzaniaweb.live