Mjiolojia Mkuu kutoka Mamlaka ya Maji Dodoma (DUWASA), Emmanuel Nahozya amesema kuwa utafiti uliofanywa na mamlaka hiyo kwakushirikiana na wadau mbalimbali umeabaini hakuna dalili yoyote ya kupungua kwa maji yaliyopo chini ya ardhi katika jiji hilo.
Nahozya ambaye anatokea katika Idara ya Rasilimali za Maji DUWASA amesema hayo mkoani humo alipokuwa anawasilisha Tathimini ya Utunzaji wa Rasilimali za Maji katika jiji hilo.
“Kulingana na wingi na ongezeko la watu katika jiji hili tumetafuata vyanzo vingine vya maji ambavyo vitatumika na hivi vilivyopo ili kuongeza uzalishaji maji katika jiji hili ili kuendana na kasi ya matumizi ya maji, amesema Nahozya.