Tue, 25 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dkt. Festo Dugange leo Julai 25 ameonekana katika Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa tangu alipopata ajali usiku wa Aprili 26 mwaka huu.
Dk. Dugange ameonekana akisalimiana na viongozi wengine wa Serikali katika viwanja hivyo vya mashujaa.
Itakumbukwa kuwa mnamo usiku wa Aprili 26 mwaka huu, Naibu Waziri huyo alipata ajali ya gari akiwa Jijini Dodoma.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live