Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dk Bashiru ataka vijana wa kimasai kudumisha mila na desturi zao

65840 Wamasai+pic

Sun, 7 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi  (CCM), Dk Bashiru Ally  amewataka vijana  wa jamii ya Kimasai  kuiunganisha jamii yao kwa kudumisha mila na desturi .

Dk Bashiru amesema hayo leo Jumamosi Julai 6, 2019 katika sherehe ya uzinduzi wa boma la Eunoto katika Kijiji cha Mti  mmoja   wilayani Monduli huku pia akitaka kudumisha  nidhamu  ili kupata maendeleo.

Amesema ili kutetea maslahi ya jamii ya wafugaji, Serikali pia inapaswa kuweka ulinzi katika maeneo ya malisho ya mifugo yao yasivamiwe.

Hata hivyo, amewashukuru Rais John Magufuli na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta kwa kutangaza undugu kati ya Kenya na   kuwataka wananchi wake wafanye biashara kwa amani.

Mkuu wa  viongozi wa Mila ya Kimasai, (Laigwanani) Lekisongo Meijo amesema Eunoto ni sherehe  ya kimila ambayo inasimika viongozi wa vijana wa kimila wa jamii hiyo.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoani Arusha,  Loota Erasto Sanare ameiomba Serikali iisaidie jamii ya wafugaji kwa kuwapatia chakula kwa bei ya chini kwa sababu si wafugaji wote wanaojishughulisha  na kilimo.

Pia Soma

 

Chanzo: mwananchi.co.tz