Tue, 23 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Diwani wa Kata ya Kunduchi jijini Dar es Salaam, Michael Urio (CCM) amesema hawezi kukubali shule iliyokumbwa na mafuriko ifunguliwe kabla mazingira yake hayajawa mazuri.
Shule hiyo inayofahamika kwa jina la Michael Urio inayofundisha michepuo ya kiingereza imepata athari hiyo baada ya mvua kubwa kunyesha kwa siku mbili mfululizo (Januari 20 na 21, 2024).
Amesema kufunguliwa kwa shule hiyo wakati hali ya mafuriko bado ipo kunaweza kusababisha wanafunzi kupata magonjwa ya milipuko.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live