Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dhahabu ya kinyemela yachukua uhai wa Wachimbaji saba

WACHIMBAJI Dhahabu ya kinyemela yachukua uhai wa Wachimbaji saba

Sun, 12 Mar 2023 Chanzo: dar24

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha vifo vya Wachimbaji wadogo saba ambao wamefariki baada ya shimo waliloingia kwa ajili ya kazi yao kujaa maji.

Kamanda Jongo amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia hii leo Machi 11, 2023 katika Kijiji cha Igando, kilichopo Kata ya Magenge Wilaya na Mkoa wa Geita.

Amesema, wachimbaji hao waliingia katika eneo lililofungwa kwa sababu za kiusalama na uwepo wa mvua za masika lakini waliingia kinyemela majira ya usiku, na tayari miili ya wachimbaji wote imeopolewa na kutambuliwa.

Aidha ameongeza kuwa, “migodi ambayo haikuwa vizuri kiusalama na hizi mvua zinazonyesha mashimo yalijaa maji, walikuwa wanaingia usiku wakazidiwa na maji wakashindwa kutoka na kupelekea umauti wao.”

Chanzo: dar24