Mon, 22 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Daraja la Kunduchi Mtongani Jijini la Dar es salaam limeanza kupitika leo baada ya juhudi za Serikali kufanya kazi usiku na mchana kurudisha mawasiliano katika eneo hilo.
Mawasiliano darajani hapo yalikatika kutokana na kipande cha barabara kinachounganika na daraja kukatika kutokana na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia juzi maeneo mbalimbali ya Dar es salaam.
Wakazi wa Mbweni, Ununio, Bahari Beach na maeneo ya jirani sasa wameanza kupita darajani hapo baada ya awali kulazimika kutumia barabara ya uelekeo wa Tegeta Nyuki na njia nyingine mbadala.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live