Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Dar, Mwanza vinara msongamano wa watu mwaka 2018

62514 Mwakapic

Thu, 13 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Dar es Salaam na Mwanza ni kati ya mikoa minne iliyotajwa kuwa na msongamano mkubwa zaidi wa watu mwaka 2018.

Mikoa mingine inayofuatia kwa idadi kubwa ya watu ni Kagera na Kilimanjaro, huku Mkoa wa Lindi ukiwa na idadi ndogo zaidi.

Hayo yameelezwa bungeni leo Alhamisi, Juni 13, 2019  na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango  alipokuwa anawasilisha taarifa ya hali ya uchumi wa Taifa  mwaka 2018 na mpango wa maendeleo wa Taifa wa mwaka 2019/20.

“Dar es Salaam ilikuwa na msongamano mkubwa zaidi wa watu…watu 3,695 kwa kila kilomita moja ya mraba ukifuatiwa na Mwanza (watu 373.1), Kagera (watu 119.6) na Kilimanjaro watu 104,” amesema Dk Mpango.

Mkoa wa Lindi amesema ulikuwa na idadi ndogo zaidi ya watu kwa kilomita moja ya mraba ikiwa na wastani wa watu 14.9, ukifuatiwa na Katavi (watu 16.1) na Ruvuma watu 24.8 kwa kila kilomita moja ya mraba.

Habari zinazohusiana na hii

Chanzo: mwananchi.co.tz