Moshi. Madereva wa daladala zinazotoa huduma ya usafirishaji katika manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro wamesitisha kutoa huduma ya usafiri kwa maelezo kuwa hawataki kuziona bajaj katika eneo lao la biashara.
Hali hiyo imesababisha adha ya usafiri kwa wakazi wa Moshi kuanzia leo asubuhi Jumatatu Desemba 3, 2018.
Akizungumza na Mwananchi leo ofisa mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti, Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), John Makwale amesema hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sasa kwa kuwa yupo kikaoni.
"Nitafute baadaye niko kwenye kikao "amesema.
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi