MKUU wa wilaya ya Arusha ,Kenani Kihongosi amekabidhi Sh milioni 5.3 kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Sinon Jijini Arusha, Nteles Lorna kwa ajili ya kutengeneza viti vipya 108 vilivyouzwa kama chuma chakavu kwa wafanyabiashara
Akikabidhi fedha hizo jana ofisini kwake, Kihongosi aliwaonya wafanyabiashara wa vyuma chakavu kuacha tabia ya kununua vitu ambavyo ni mali ya serikali.
Alisema fedha hizo zimechangwa na wazazi, walezi wa watoto pamoja na wafanyabiashara wa vyuma chakavu na kuongeza kuwa serikali inatoa fedha nyingi kuhakikisha watoto wanapata elimu hivyo kitendo cha kuiba viti ni cha kusikitisha na ni uhujumu uchumi.
Aliwataka pia watendaji wa kata ,wajumbe wa serikali za mtaa na mwenyeviti wa mtaa kuhakikisha watoto wanaokuwa mitaani wanakwenda shule kwa sababu wazazi wanawatumia kwenda kuuza vyuma.