Wakazi wa mtaa wa Idundilanga Halmashauri ya mji wa Njombe wameitaka serikali kutoa ufafanuzi kuhusu kuanza ujenzi wa Uwanja wa ndege uliopo mjini humo ili kuwaepusha na kero inayowatesa muda wote ya kukabwa na vibaka
Wakitoa kero zao katika mkutano ,wakazi wamesema wanapata shida kubwa kwasababu kukosekana kwa vituo vya basi katikati ya mji pamoja na kukamatwa na kulipishwa faini kwasababu ya kukatisha katika uwanja wa ndege uliyopo mjini Njombe ambao wanasema hautumika ipasavyo na ndege hivyo wanaomba serikali ione namna ya kutatua adha hizo.
Akijibu kero hizo Mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Gwakisa Kasongwa amesema tayari serikali imekamilisha mchakato wa awali ujenzi wa uwanja wa ndege wa mkoa wa Njombe na kisha kutoa onyo kwa wanaotumia uwanja huo kinyume na taratibu kwasababu ni kosa kisheria .
Aidha mkuu wa wilaya ya Njombe ametoa onyo kwa watendaji wazembe wanaoshindwa kutekeleza maagizo ya serikali ,kwamba haitasita kuwapeleka pembezoni mwa miji na kuwaleta mijini wanaofanya kazi kwa bidii ili kujifunza kwao.