Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DC Ole Sabaya akakabidhi fedha za ada wanafunzi chuo cha ualimu ‘zilizokwapuliwa’

78229 Sabayapic

Thu, 3 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Hai. Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya  amemaliza mgogoro wa upotevu wa  fedha kiasi cha Sh76.9 milioni za  wanafunzi wa Chuo cha Ualimu Moshi uliodumu zaidi ya mwaka mmoja.

Akizungumza leo Jumatano Oktoba 2,2019  Sabaya amesema tayari Sh56 milioni zimeshatolewa na wahusika na kwamba, wanafunzi  wataendelea na masomo bila kikwazo.

Amesema  wahusika waliokuwa wanadaiwa fedha hizo ni aliyekuwa  mweka hazina wa chuo hicho Sarafina Mbwambo ambaye amelipa  Sh10 milioni kati ya Sh20 milioni anazotakiwa kuzilipa.

Wengine waliorejesha  ni wakala wa  benki ya  CRDB kupitia  Saccos ELCT, Melkizedeck Mchau ambaye amelipa Sh20milioni  kiasi chote ambacho alitakiwa kulipa.

Pia, chuo hicho  kimelipa Sh12.3 milioni na benki ya CRDB imeahidi kulipa deni wanalotakiwa  kulipa  ndani ya wiki mbili kuanzia leo a ni Sh12.3milioni.

Naye  Mkurugenzi wa chuo hicho, Joseph Mong'are alimshukuru Rais John Magufuli kwa jitihada za kuhakikisha fedha za wazazi wanyonge zinarudishwa kwa kuzingatia haki na usawa.

Pia Soma

Advertisement
 

Chanzo: mwananchi.co.tz