Mkuu wa wilaya ya Longido Mhe Marco H. Ng'umbi tarehe 26/11/2023 alifunga mafunzo ya awali ya jeshi la akiba katika kata ya Mundarara wilayani longido, Katika sherehe hiyo ya kufunga mafunzo Mkuu wa wilaya amewapongeza vijana wote waliomaliza kwa kuwa na uvumilivu na nidhamu katika kipindi chote cha mafunzo.
Mkuu wa wilaya ya Longido Mhe Marco H. Ng'umbi tarehe 26/11/2023 alifunga mafunzo ya awali ya jeshi la akiba katika kata ya Mundarara wilayani longido, Katika sherehe hiyo ya kufunga mafunzo Mkuu wa wilaya amewapongeza vijana wote waliomaliza kwa kuwa na uvumilivu na nidhamu katika kipindi chote cha mafunzo. Katika hotuba yake amewaasa vijana hao kuendelea Kuiheshimu, kuilinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kutii Serikali na Rais wake ambaye ndio Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Ulinzi na usalama Dkt @Samia_Suluhu_Hassan, na pia kutojiingiza kwenye makundi mabaya.