Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

DC Jerry Muro ampongeza Magufuli kuwateua vijana

27870 Pic+muro TanzaniaWeb

Tue, 20 Nov 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Mkuu wa wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, Jerry Muro amesema Serikali ya Tanzania imepiga hatua katika kuwawezesha vijana kwa kuwapa nafasi mbalimbali za uongozi serikalini.

Muro amesema hayo leo Jumatatu Novemba 19, 2018 wakati akitoa salamu za Serikali kwenye mkutano wa pili wa mwaka wa vijana katika nchi za Afrika Mashariki unaofanyika katika kituo cha MS TCDC.

"Rais John Magufuli ameonyesha imani kubwa kwa kuwaamini vijana na amewateua kushika nyadhifa zikiwemo mawaziri, naibu mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya," amesema Muro.

Muro hata hivyo, amekemea tabia ya vijana kutumia teknolojia ya mawasiliano vibaya kwa kuweka picha zisizo na maadili badala ya kuchangamkia fursa hiyo kutangaza biashara na kazi za ubunifu.



Chanzo: mwananchi.co.tz